Swahili New Testament Bible

Titus 3

Philemon

Return to Index

Chapter 1

1


 

  Mimi Paulo, mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu, na ndugu Timotheo, ninakuandikia wewe Filemoni mpendwa, mfanyakazi mwenzetu  

 

 

-

2


 

  na kanisa linalokutana nyumbani kwako, na wewe dada Afia, na askari mwenzetu Arkupo.  

 

 

-

3


 

  Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana yesu Kristo.  

 

 

-

4


 

  Kila wakati ninaposali nakukumbuka wewe Filemoni, na kumshukuru Mungu  

 

 

-

5


 

  maana nasikia habari za imani yako kwa Bwana wetu Yesu na upendo wako kwa watu wote wa Mungu.  

 

 

-

6


 

  Naomba ili imani hiyo unayoshiriki pamoja nasi ikuwezeshe kuwa na ujuzi mkamilifu zaidi wa baraka zote tunazopata katika kuungana kwetu na Kristo.  

 

 

-

7


 

  Ndugu, upendo wako yameniletea furaha kubwa na kunipa moyo sana! Nawe umeichangamsha mioyo ya watu wa Mungu.  

 

 

-

8


 

  Kwa sababu hiyo, ningeweza, kwa uhodari kabisa, nikiwa ndugu yako katika Kristo, kukuamuru ufanye unachopaswa kufanya.  

 

 

-

9


 

  Lakini kwa sababu ya upendo, ni afadhali zaidi nikuombe. Nafanya hivi ingawa mimi ni Paulo, balozi wa Kristo Yesu, na sasa pia mfungwa kwa ajili yake.  

 

 

-

10


 

  Basi, ninalo ombi moja kwako kuhusu mwanangu Onesimo, ambaye ni mwanangu katika Kristo kwani nimekuwa baba yake nikiwa kifungoni.  

 

 

-

11


 

  Ni Onesimo yuleyule ambaye wakati mmoja alikuwa hakufai kitu, lakini sasa ananifaa mimi na wewe pia.  

 

 

-

12


 

  Sasa namrudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe.  

 

 

-

13


 

  Ningependa akae nami hapa anisaidie badala yako wakati niwapo kifungoni kwa sababu ya Habari Njema.  

 

 

-

14


 

  Lakini sitafanya chochote bila kibali chako. Sipendi kukulazimisha unisaidie, kwani wema wako unapaswa kutokana na hiari yako wewe mwenyewe na si kwa kulazimika.  

 

 

-

15


 

  Labda Onesimo aliondoka kwako kwa kitambo tu, kusudi uweze tena kuwa naye daima.  

 

 

-

16


 

  Na sasa yeye si mtumwa tu, ila ni bora zaidi ya mtumwa: yeye ni ndugu yetu mpenzi. Na wa maana sana kwangu mimi, na kwako atakuwa wa maana zaidi kama mtumwa na kama ndugu katika Bwana.  

 

 

-

17


 

  Basi, ikiwa wanitambua mimi kuwa mwenzako, mpokee tena kama vile ungenipokea mimi mwenyewe.  

 

 

-

18


 

  Kama alikuwa amekukosea kitu, au alikuwa na deni lako, basi, unidai mimi.  

 

 

-

19


 

  Naandika jambo hili kwa mkono wangu mwenyewe: yako.)  

 

 

-

20


 

  Haya, basi, ndugu yangu, nifanyie jambo hilo kwa ajili ya jina la Bwana; burudisha moyo wangu kama ndugu katika Kristo.  

 

 

-

21


 

  Naandika nikitumaini kwamba utanikubalia ombi langu; tena najua kwamba utafanya hata zaidi ya haya ninayokuomba.  

 

 

-

22


 

  Pamoja na hayo, nitayarishie chumba kwani natumaini kwamba kwa sala zenu, Mungu atanijalia niwatembeleeni.  

 

 

-

23


 

  Epafra, mfungwa mwenzangu kwa ajili ya Kristo Yesu, anakusalimu.  

 

 

-

24


 

  Nao akina Marko, Aristarko, Dema na Luka, wafanyakazi wenzangu, wanakusalimu.  

 

 

-

25


 

  Nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.  

 

 

-

Hebrews 1

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: