Swahili New Testament Bible

1st Timothy 1

1 Timothy

Return to Index

Chapter 2

1


 

  Kwanza kabisa, basi naomba dua, sala, maombi na sala za shukrani zitolewe kwa Mungu kwa ajili ya watu wote,  

 

 

-

2


 

  kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani pamoja na uchaji wa Mungu na mwenendo mwema.  

 

 

-

3


 

  Jambo hili ni jema na lampendeza Mungu Mwokozi wetu,  

 

 

-

4


 

  ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli.  

 

 

-

5


 

  Maana yuko Mungu mmoja, na pia yuko mmoja anayewapatanisha watu na Mungu, binadamu Kristo Yesu,  

 

 

-

6


 

  ambaye alijitoa mwenyewe kuwakomboa watu wote. Huo ulikuwa uthibitisho, wakati ufaao ulipowadia.  

 

 

-

7


 

  Kwa sababu hiyo mimi nilitumwa niwe mtume na mwalimu wa watu wa mataifa, niutangaze ujumbe wa imani na ukweli. Nasema ukweli; sisemi uongo!  

 

 

-

8


 

  Basi, popote mnapokutana kufanya ibada nataka wanaume wasali, watu waliojitolea kweli na ambao wanaweza kuinua mikono yao wakisali bila hasira wala ubishi.  

 

 

-

9


 

  Hali kadhalika, nawataka wanawake wawe wanyofu na wenye busara kuhusu mavazi yao; wavae sawasawa na si kwa urembo wa mitindo ya kusuka nywele, kujipamba kwa dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,  

 

 

-

10


 

  bali kwa matendo mema kama iwapasavyo wanawake wamchao Mungu.  

 

 

-

11


 

  Wanawake wanapaswa kukaa kimya na kuwa wanyenyekevu wakati wa kujifunza.  

 

 

-

12


 

  Mimi simruhusu mwanamke amfundishe au amtawale mwanamume; anapaswa kukaa kimya.  

 

 

-

13


 

  Maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa.  

 

 

-

14


 

  Na wala si Adamu aliyedanganywa; bali mwanamke ndiye aliyedanganywa, akaivunja sheria ya Mungu.  

 

 

-

15


 

  Hata hivyo, mwanamke ataokolewa kwa kupata watoto, kama akidumu katika imani, upendo, utakatifu na unyofu.  

 

 

-

1st Timothy 3

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: