Swahili New Testament Bible

1st Thessalonians 3

1 Thessalonians

Return to Index

Chapter 4

1


 

  Hatimaye, ndugu zangu, mmejifunza kutoka kwetu namna mnavyopaswa kuishi ili kumpendeza Mungu. Na kweli mmekuwa mnaishi hivyo. Sasa tunawaombeni na kuwasihi kwa jina la Bwana Yesu mfanye vema zaidi.  

 

 

-

2


 

  Maana mnayajua yale maagizo tuliyowapeni kwa mamlaka ya Bwana Yesu.  

 

 

-

3


 

  Mungu anataka ninyi muwe watakatifu na mjiepushe kabisa na maisha ya zinaa.  

 

 

-

4


 

  Kila mwanamume anapaswa kujua namna ya kuishi na mkewe kwa utakatifu na heshima,  

 

 

-

5


 

  na si kwa tamaa mbaya kama watu wa mataifa mengine wasiomjua Mungu.  

 

 

-

6


 

  Basi, mtu yeyote asimkosee au kumpunja mwenzake kuhusu jambo hili. Tulikwisha waambieni hayo na kuwaonya kwamba Bwana atawaadhibu wanaofanya mambo hayo.  

 

 

-

7


 

  Mungu hakutuita tuishi maisha ya zinaa, bali tuishi katika utakatifu.  

 

 

-

8


 

  Kwa hiyo basi, anayedharau mafundisho hayo hamdharau mtu, bali amdharau Mungu mwenyewe anayewapeni Roho wake Mtakatifu.  

 

 

-

9


 

  Hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya kuwapenda ndugu zenu waumini. Ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu namna mnavyopaswa kupendana.  

 

 

-

10


 

  Na mmekuwa mkiwatendea hivyo ndugu zenu wote kila mahali katika Makedonia. Basi, ndugu tunawaombeni mfanye hata zaidi.  

 

 

-

11


 

  Muwe na nia ya kuishi maisha ya utulivu, kila mmoja ashughulikie mambo yake mwenyewe na afanye kazi kwa mikono yake mwenyewe kama tulivyowaagiza pale awali.  

 

 

-

12


 

  Kwa namna hiyo mtajipatia sifa nzuri kutoka kwa wale wasio Wakristo, na hamtakuwa na lazima ya kuwategemea wengine kwa mahitaji yenu.  

 

 

-

13


 

  Ndugu, twataka mjue ukweli kuhusu wale ambao wamekwisha fariki dunia, ili msipatwe na huzuni kama watu wengine wasio na matumaini.  

 

 

-

14


 

  Sisi tunaamini kwamba Yesu alikufa, akafufuka; na hivyo sisi tunaamini kwamba Mungu atawaleta pamoja na Yesu wale wote waliofariki wakiwa wanamwamini.  

 

 

-

15


 

  Hili tunalowaambieni ni fundisho la Bwana; sisi tulio hai, ambao tutakuwa tumebaki, wakati Bwana atakapokuja, hakika hatutawatangulia wale waliokwisha fariki dunia.  

 

 

-

16


 

  Maana patatolewa amri, sauti ya malaika mkuu, sauti ya tarumbeta ya Mungu, naye Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni. Ndipo wale waliokufa wakiwa wanamwamini Kristo watafufuliwa kwanza.  

 

 

-

17


 

  Kisha sisi tulio hai wakati huo tutakusanywa pamoja nao katika mawingu kumlaki Bwana hewani. Na hivyo tutakuwa daima pamoja na Bwana.  

 

 

-

18


 

  Basi, farijianeni kwa maneno haya.  

 

 

-

1st Thessalonians 5

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: