Swahili New Testament Bible

Ephesians 4

Ephesians

Return to Index

Chapter 5

1


 

  Kwa hiyo, mwigeni Mungu, maana ninyi ni watoto wake wapenzi.  

 

 

-

2


 

  Upendo uongoze maisha yenu, kama vile Kristo alivyotupenda, na kwa ajili yetu akajitoa mwenyewe kama dhabihu yenye harufu nzuri na tambiko impendezayo Mungu.  

 

 

-

3


 

  Kwa vile ninyi ni watu wa Mungu, basi uasherati, uchafu wowote ule au choyo visitajwe kamwe miongoni mwenu.  

 

 

-

4


 

  Tena maneno ya aibu, ya upuuzi au ubishi, yote hayo hayafai kwenu; maneno ya kumshukuru Mungu ndiyo yanayofaa.  

 

 

-

5


 

  Jueni wazi kwamba mwasherati yeyote au mchafu au mfisadi, (ufisadi ni sawa na kuabudu sanamu), au mtu yeyote wa aina hiyo hataambulia chochote katika Utawala wa Kristo na wa Mungu.  

 

 

-

6


 

  Msikubali kudanganywa na mtu kwa maneno matupu; maana, kwa sababu ya mambo kama hayo ghadhabu ya Mungu huwajia wote wasiomtii.  

 

 

-

7


 

  Basi, msishirikiane nao.  

 

 

-

8


 

  Zamani ninyi mlikuwa gizani, lakini sasa ninyi mko katika mwanga kwa kuungana na Bwana. Ishini kama watoto wa mwanga:  

 

 

-

9


 

  maana matokeo ya mwanga ni wema kamili, uadilifu na ukweli.  

 

 

-

10


 

  Jaribuni kujua yale yanayompendeza Bwana.  

 

 

-

11


 

  Msishiriki katika matendo yasiyofaa, ya giza bali yafichueni.  

 

 

-

12


 

  Mambo yanayotendwa kwa siri ni aibu hata kuyataja.  

 

 

-

13


 

  Lakini mambo yale yanayotendwa katika mwanga, ukweli wake hudhihirishwa;  

 

 

-

14


 

  na kila kilichodhihirishwa huwa mwanga. Ndiyo maana Maandiko yasema: "Amka wewe uliyelala, fufuka kutoka wafu, naye Kristo atakuangaza."  

 

 

-

15


 

  Basi, muwe waangalifu jinsi mnavyoishi: Msiishi kama wapumbavu, bali kama wenye hekima.  

 

 

-

16


 

  Tumieni vizuri muda mlio nao maana siku hizi ni mbaya.  

 

 

-

17


 

  Kwa hiyo, msiwe wapumbavu, bali jaribuni kujua matakwa ya Bwana.  

 

 

-

18


 

  Acheni kulewa divai maana hiyo itawaangamiza, bali mjazwe Roho Mtakatifu.  

 

 

-

19


 

  Zungumzeni kwa maneno ya Zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Bwana nyimbo na zaburi kwa shukrani mioyoni mwenu.  

 

 

-

20


 

  Mshukuruni Mungu Baba daima kwa ajili ya yote, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.  

 

 

-

21


 

  Kila mmoja amstahi mwenzake kwa sababu ya kumcha Kristo.  

 

 

-

22


 

  Wake wawatii waume zao kama kumtii Bwana.  

 

 

-

23


 

  Maana mume anayo mamlaka juu ya mkewe, kama vile Kristo alivyo na mamlaka juu ya kanisa; naye Kristo mwenyewe hulikomboa kanisa, mwili wake.  

 

 

-

24


 

  Kama vile kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo, wake wawatii waume zao katika mambo yote.  

 

 

-

25


 

  Nanyi waume, wapendeni wake zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa, akajitoa mwenyewe sadaka kwa ajili yake.  

 

 

-

26


 

  Alifanya hivyo, ili kwa neno lake, aliweke wakfu kwa Mungu, baada ya kulifanya safi kwa kuliosha katika maji,  

 

 

-

27


 

  kusudi ajipatie kanisa lililo takatifu na safu kabisa, kanisa lisilo na doa, kasoro au chochote cha namna hiyo.  

 

 

-

28


 

  Basi, waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. ((  

 

 

-

29


 

  Hakuna mtu yeyote auchukiaye mwili wake; badala ya kuuchukia, huulisha na kuuvika. Ndivyo naye Kristo anavyolitunza kanisa,  

 

 

-

30


 

  maana sisi ni viungo vya mwili wake.)  

 

 

-

31


 

  Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Kwa hiyo, mwanamume atawaacha baba na mama yake, ataungana na mkewe, nao wawili watakuwa mwili mmoja."  

 

 

-

32


 

  Kuna ukweli uliofichika katika maneno haya, nami naona kwamba yamhusu Kristo na kanisa lake.  

 

 

-

33


 

  Lakini yanawahusu ninyi pia: kila mume lazima ampende mkewe kama nafsi yake mwenyewe, naye mke anapaswa kumstahi mumewe.  

 

 

-

Ephesians 6

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: