Swahili New Testament Bible

Galatians 5

Galatians

Return to Index

Chapter 6

1


 

  Ndugu, kama mkimwona mtu fulani amekosea, basi, ninyi mnaoongozwa na Roho mwonyeni mtu huyo ajirekebishe; lakini fanyeni hivyo kwa upole, mkiwa na tahadhari msije nanyi wenyewe mkajaribiwa.  

 

 

-

2


 

  Saidianeni kubeba mizigo yenu na hivyo mtatimiza sheria ya Kristo.  

 

 

-

3


 

  Mtu akijiona kuwa ni kitu, na kumbe si kitu, huyo anajidanganya mwenyewe.  

 

 

-

4


 

  Lakini kila mmoja na aupime vizuri mwenendo wake mwenyewe. Ukiwa mwema, basi, anaweza kuona fahari juu ya alichofanya bila kuwa na sababu ya kujilinganisha na mtu mwingine.  

 

 

-

5


 

  Maana kila mmoja anao mzigo wake mwenyewe wa kubeba.  

 

 

-

6


 

  Mwenye kufundishwa neno la Mungu na amshirikishe mwalimu wake riziki zake.  

 

 

-

7


 

  Msidanganyike; Mungu hafanyiwi dhihaka. Alichopanda mtu ndicho atakachovuna.  

 

 

-

8


 

  Apandaye katika tamaa za kidunia, atavuna humo uharibifu; lakini akipanda katika Roho, atavuna kutoka kwa Roho uzima wa milele.  

 

 

-

9


 

  Basi, tusichoke kutenda mema; maana tusipolegea tutavuna mavuno kwa wakati wake.  

 

 

-

10


 

  Kwa hiyo, tukiwa bado na wakati, tuwatendee watu wote mema, na hasa ndugu wa imani yetu.  

 

 

-

11


 

  Tazameni jinsi nilivyoandika kwa herufi kubwa, kwa mkono wangu mwenyewe.  

 

 

-

12


 

  Wale wanaotaka kuonekana wazuri kwa mambo ya mwili ndio wanaotaka kuwalazimisha ninyi mtahiriwe. Wanafanya hivyo kwa sababu moja tu: kusudi wao wenyewe wasije wakadhulumiwa kwa sababu ya msalaba wa Kristo.  

 

 

-

13


 

  Maana, hao wenyewe waliotahiriwa hawaishiki Sheria; huwataka ninyi mtahiriwe wapate kujivunia alama hiyo mwilini mwenu.  

 

 

-

14


 

  Lakini mimi sitajivunia kamwe chochote isipokuwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo; maana kwa njia ya msalaba huo ulimwengu umesulubiwa kwangu, nami nimesulubiwa kwa ulimwengu.  

 

 

-

15


 

  Kutahiriwa au kutotahiriwa si kitu; cha maana ni kuwa kiumbe kipya.  

 

 

-

16


 

  Wanaoufuata mwongozo huo nawatakia amani na huruma; amani na huruma kwa Israeli--Wateule wa Mungu.  

 

 

-

17


 

  Basi, sasa mtu yeyote asinisumbue tena, maana alama nilizo nazo mwilini mwangu ni zile za Yesu.  

 

 

-

18


 

  Ndugu, nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Kristo. Amina.  

 

 

-

Ephesians 1

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: