Swahili New Testament Bible

1st Corinthians 15

1 Corinthians

Return to Index

Chapter 16

1


 

  Sasa, yahusu ule mchango kwa ajili ya watu wa Mungu: fanyeni kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia.  

 

 

-

2


 

  Kila Jumapili kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha kadiri ya mapato yake, ili kusiwe na haja ya kufanya mchango wakati nitakapokuja.  

 

 

-

3


 

  Wakati nitakapokuja kwenu, nitawatuma wale mtakaowachagua miongoni mwenu wapeleke barua na zawadi zenu Yerusalemu.  

 

 

-

4


 

  Kama itafaa nami niende, basi, watakwenda pamoja nami.  

 

 

-

5


 

  Nitakuja kwenu, baada ya kupitia Makedonia--maana nataraji kupitia Makedonia.  

 

 

-

6


 

  Labda nitakaa kwenu kwa muda fulani, au huenda nitakaa pamoja nanyi wakati wote wa baridi, ili mpate kunisaidia niendelee na safari yangu kokote nitakakokwenda.  

 

 

-

7


 

  Sipendi kupita kwenu harakaharaka na kuendelea na safari. Natumaini kukaa kwenu kwa kitambo fulani, Bwana akiniruhusu.  

 

 

-

8


 

  Lakini nitabaki hapa Efeso mpaka siku ya Pentekoste.  

 

 

-

9


 

  Mlango uko wazi kabisa kwa ajili ya kazi yangu muhimu hapa, ingawa wapinzani nao ni wengi.  

 

 

-

10


 

  Timotheo akija, angalieni asiwe na hofu yoyote wakati yupo kati yenu, kwani anafanya kazi ya Bwana kama mimi.  

 

 

-

11


 

  Kwa hiyo mtu yeyote asimdharau, ila msaidieni aendelee na safari yake kwa amani ili aweze kurudi kwangu, maana mimi namngojea pamoja na ndugu zetu.  

 

 

-

12


 

  Kuhusu ndugu Apolo, nimemsihi sana aje kwenu pamoja na ndugu wengine, lakini hapendelei kabisa kuja sasa ila atakuja mara itakapowezekana.  

 

 

-

13


 

  Kesheni, simameni imara katika imani, muwe hodari na wenye nguvu.  

 

 

-

14


 

  Kila mfanyacho kifanyike kwa upendo.  

 

 

-

15


 

  Ndugu, mnaifahamu jamaa ya Stefana; wao ni watu wa kwanza kabisa kuipokea imani ya Kikristo katika Akaya, na wamejitolea kuwatumikia watu wa Mungu. Ninawasihi ninyi ndugu zangu,  

 

 

-

16


 

  muufuate uongozi wa watu kama hao, na uongozi wa kila mtu afanyaye kazi na kutumikia pamoja nao.  

 

 

-

17


 

  Nafurahi sana kwamba Stefana, Fortunato na Akaiko wamefika; wamelijaza pengo lililokuwako kwa kutokuwako kwenu.  

 

 

-

18


 

  Wameiburudisha roho yangu na yenu pia. Kwa hiyo inafaa kuwakumbuka watu wa namna hii.  

 

 

-

19


 

  Makanisa yote ya Asia yanawasalimuni. Akula na Priskila pamoja na watu wote wa Mungu walio nyumbani mwao wanawasalimuni sana katika Bwana.  

 

 

-

20


 

  Ndugu wote wanawasalimuni. Nanyi salimianeni kwa ishara ya mapendo ya Mungu.  

 

 

-

21


 

  Mimi Paulo nawasalimuni, nikiandika kwa mkono wangu mwenyewe.  

 

 

-

22


 

  Yeyote asiyempenda Bwana, na alaaniwe. MARANA THA--BWANA, njoo!  

 

 

-

23


 

  Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.  

 

 

-

24


 

  Mapendo yangu yawe kwenu katika kuungana na Kristo Yesu.  

 

 

-

2nd Corinthians 1

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: