Swahili New Testament Bible

1st Corinthians 11

1 Corinthians

Return to Index

Chapter 12

1


 

  Ndugu, kuhusu vipaji vya kiroho, napenda mfahamu vizuri mambo haya:  

 

 

-

2


 

  Mnajua kwamba, kabla ya kuongoka kwenu, mlitawaliwa na kupotoshwa na sanamu tupu.  

 

 

-

3


 

  Basi, jueni kwamba mtu yeyote anayeongozwa na Roho wa Mungu hawezi kusema: "Yesu alaaniwe!" Hali kadhalika, mtu yeyote hawezi kusema: "Yesu ni Bwana," asipoongozwa na Roho Mtakatifu.  

 

 

-

4


 

  Vipaji vya kiroho ni vya namna nyingi, lakini Roho avitoaye ni mmoja.  

 

 

-

5


 

  Kuna namna nyingi za kutumikia, lakini Bwana anayetumikiwa ni mmoja.  

 

 

-

6


 

  Kuna namna mbalimbali za kufanya kazi ya huduma, lakini Mungu ni mmoja, anayewezesha kazi zote katika wote.  

 

 

-

7


 

  Kila mtu hupewa mwangaza wa Roho kwa faida ya wote.  

 

 

-

8


 

  Roho humpa mmoja ujumbe wa hekima, na mwingine ujumbe wa elimu apendavyo Roho huyohuyo.  

 

 

-

9


 

  Roho huyohuyo humpa mmoja imani, na humpa mwingine kipaji cha kuponya;  

 

 

-

10


 

  humpa mmoja kipaji cha kufanya miujiza, mwingine kipaji cha kusema ujumbe wa Mungu, mwingine kipaji cha kubainisha vipaji vitokavyo kwa Roho na visivyo vya Roho; humpa mmoja kipaji cha kusema lugha ngeni, na mwingine kipaji cha kuzifafanua.  

 

 

-

11


 

  Hizo zote ni kazi za Roho huyohuyo mmoja, ambaye humpa kila mtu kipaji tofauti, kama apendavyo mwenyewe.  

 

 

-

12


 

  Kama vile mwili ulivyo mmoja wenye viungo vingi, na viungo hivyo vyote--ingawaje ni vingi--hufanya mwili mmoja, ndivyo ilivyo pia kwa Kristo.  

 

 

-

13


 

  Maana sisi, tukiwa Wayahudi au watu wa mataifa mengine, watumwa au watu huru, sote tumebatizwa kwa Roho mmoja katika mwili huo mmoja; na sote tukanyweshwa Roho huyo mmoja.  

 

 

-

14


 

  Mwili hauna kiungo kimoja tu, bali una viungo vingi.  

 

 

-

15


 

  Kama mguu ungejisemea: "Kwa kuwa mimi si mkono, basi mimi si mali ya mwili", je, ungekoma kuwa sehemu ya mwili? La hasha!  

 

 

-

16


 

  Kama sikio lingejisemea: "Kwa vile mimi si jicho, basi mimi si mali ya mwili", je, kwa hoja hiyo lingekoma kuwa sehemu ya mwili? La!  

 

 

-

17


 

  Kama mwili wote ungekuwa jicho, sikio lingekuwa wapi? Na kama mwili wote ungekuwa sikio, mtu angewezaje kunusa?  

 

 

-

18


 

  Lakini kama ilivyo, Mungu alizipanga sehemu hizo tofauti katika mwili kama alivyopenda.  

 

 

-

19


 

  Kama sehemu zote zingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?  

 

 

-

20


 

  Ukweli ni kwamba, sehemu za mwili ni nyingi, lakini mwili ni mmoja.  

 

 

-

21


 

  Basi, jicho haliwezi kuuambia mkono: "Sikuhitaji wewe", wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu: "Siwahitaji ninyi."  

 

 

-

22


 

  Zaidi ya hayo, inaonekana kwamba sehemu zile za mwili zinazoonekana kuwa ni dhaifu ndizo zilizo muhimu zaidi.  

 

 

-

23


 

  Tena, viungo vile tunavyovifikiria kuwa havistahili heshima kubwa, ndivyo tunavyovitunza kwa uangalifu zaidi; viungo vya mwili ambavyo havionekani kuwa vizuri sana, huhifadhiwa zaidi,  

 

 

-

24


 

  ambapo viungo vingine havihitaji kushughulikiwa. Mungu mwenyewe ameuweka mwili katika mpango, akakipa heshima zaidi kiungo kile kilichopungukiwa heshima,  

 

 

-

25


 

  ili kusiweko na utengano katika mwili bali viungo vyote vishughulikiane.  

 

 

-

26


 

  Kama kiungo kimoja kinaumia viungo vyote huumia pamoja nacho. Kiungo kimoja kikisifiwa viungo vingine vyote hufurahi pamoja nacho.  

 

 

-

27


 

  Basi, ninyi nyote ni mwili wa Kristo; kila mmoja wenu ni kiungo cha mwili huo.  

 

 

-

28


 

  Mungu ameweka katika kanisa: kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu; kisha ameweka wale wenye kipaji cha kufanya miujiza, kuponya, kusaidia; viongozi na wenye kusema lugha ngeni.  

 

 

-

29


 

  Je, wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni walimu? Wote ni wenye kipaji cha kufanya miujiza?  

 

 

-

30


 

  Je, wote ni wenye kipaji cha kuponya? Wote ni wenye kipaji cha kusema lugha ngeni? Je, wote hufafanua lugha?  

 

 

-

31


 

  Muwe basi, na tamaa ya kupata vipaji muhimu zaidi. Nami sasa nitawaonyesheni njia bora zaidi kuliko hizi zote.  

 

 

-

1st Corinthians 13

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: