Swahili New Testament Bible

John 3

John

Return to Index

Chapter 4

1


 

  Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane.  

 

 

-

2


 

  Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.)  

 

 

-

3


 

  Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya;  

 

 

-

4


 

  na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.  

 

 

-

5


 

  Basi, akafika Sukari, mji mmoja wa Samaria, karibu na shamba ambalo Yakobo alikuwa amempa mwanawe, Yosefu.  

 

 

-

6


 

  Mahali hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, naye Yesu, kutokana na uchovu wa safari, akaketi kando ya kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.  

 

 

-

7


 

  Basi, mwanamke mmoja Msamaria akafika kuteka maji. Yesu akamwambia, "Nipatie maji ninywe."  

 

 

-

8


 

  (Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)  

 

 

-

9


 

  Lakini huyo mwanamke akamwambia, "Wewe ni Myahudi; mimi ni mwanamke Msamaria! Unawezaje kuniomba maji?" (Wayahudi hawakuwa na ushirikiano na Wasamaria katika matumizi ya vitu.)  

 

 

-

10


 

  Yesu akamjibu, "Kama tu ungalijua zawadi ya Mungu na ni nani anayekwambia: `Nipatie maji ninywe,` ungalikwisha mwomba, naye angekupa maji yaliyo hai."  

 

 

-

11


 

  Huyo mama akasema, "Mheshimiwa, wewe huna chombo cha kutekea maji, nacho kisima ni kirefu; utapata wapi maji yaliyo hai?  

 

 

-

12


 

  Au, labda wewe wajifanya mkuu kuliko babu yetu Yakobo? Yeye alitupa sisi kisima hiki; na yeye mwenyewe, watoto wake na mifugo yake walikunywa maji ya kisima hiki."  

 

 

-

13


 

  Yesu akamjibu, "Kila anayekunywa maji haya ataona kiu tena.  

 

 

-

14


 

  Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa milele."  

 

 

-

15


 

  Huyo mwanamke akamwambia, "Mheshimiwa, nipe maji hayo ili nisione kiu tena; nisije tena mpaka hapa kuteka maji."  

 

 

-

16


 

  Yesu akamwambia, "Nenda ukamwite mumeo uje naye hapa."  

 

 

-

17


 

  Huyo mwanamke akamwambia, "Mimi sina mume." Yesu akamwambia, "Umesema kweli, kwamba huna mume.  

 

 

-

18


 

  Maana umekuwa na waume watano, na huyo unayeishi naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli."  

 

 

-

19


 

  Huyo Mwanamke akamwambia, "Mheshimiwa, naona ya kuwa wewe u nabii.  

 

 

-

20


 

  Babu zetu waliabudu juu ya mlima huu, lakini ninyi mwasema kwamba mahali pa kumwabudu Mungu ni kule Yerusalemu."  

 

 

-

21


 

  Yesu akamwambia, "Niamini; wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba juu ya mlima huu, wala kule Yerusalemu.  

 

 

-

22


 

  Ninyi Wasamaria mnamwabudu yule msiyemjua, lakini sisi tunamjua huyo tunayemwabudu, kwa maana wokovu unatoka kwa Wayahudi.  

 

 

-

23


 

  Lakini wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wanaoabudu kweli, watamwabudu Baba kwa nguvu ya Roho; watu wanaomwabudu hivyo ndio Baba anaotaka.  

 

 

-

24


 

  Mungu ni Roho, na watu wataweza tu kumwabudu kweli kwa nguvu ya Roho wake."  

 

 

-

25


 

  Huyo mama akamwambia, "Najua kwamba Masiha, aitwaye Kristo, anakuja. Atakapokuja atatujulisha kila kitu."  

 

 

-

26


 

  Yesu akamwambia, "Mimi ninayesema nawe, ndiye."  

 

 

-

27


 

  Hapo wanafunzi wake wakarudi, wakastaajabu sana kuona anaongea na mwanamke. Lakini hakuna mtu aliyesema: "Unataka nini?" au, "Kwa nini unaongea na mwanamke?"  

 

 

-

28


 

  Huyo mama akauacha mtungi wake pale, akaenda mjini na kuwaambia watu,  

 

 

-

29


 

  "Njoni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyotenda! Je, yawezekana kuwa yeye ndiye Kristo?"  

 

 

-

30


 

  Watu wakatoka mjini, wakamwendea Yesu.  

 

 

-

31


 

  Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: "Mwalimu, ule chakula."  

 

 

-

32


 

  Lakini Yesu akawaambia, "Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi."  

 

 

-

33


 

  Wanafunzi wake wakaulizana, "Je, kuna mtu aliyemletea chakula?"  

 

 

-

34


 

  Yesu akawaambia, "Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake.  

 

 

-

35


 

  Ninyi mwasema: `Bado miezi minne tu, na wakati wa mavuno utafika!` Lakini mimi nawaambieni, yatazameni mashamba; mazao yako tayari kuvunwa.  

 

 

-

36


 

  Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja.  

 

 

-

37


 

  Kwa sababu hiyo msemo huu ni kweli: `Mmoja hupanda na mwingine huvuna.`  

 

 

-

38


 

  Mimi nimewatuma mkavune mavuno ambayo hamkuyatolea jasho, wengine walifanya kazi, lakini ninyi mnafaidika kutokana na jasho lao."  

 

 

-

39


 

  Wasamaria wengi wa kijiji kile waliamini kwa sababu ya maneno aliyosema huyo mama: "Ameniambia mambo yote niliyofanya."  

 

 

-

40


 

  Wasamaria walimwendea Yesu wakamwomba akae nao; naye akakaa hapo siku mbili.  

 

 

-

41


 

  Watu wengi zaidi walimwamini kwa sababu ya ujumbe wake.  

 

 

-

42


 

  Wakamwambia yule mama, "Sisi hatuamini tu kwa sababu ya maneno yako; sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba huyu ndiye kweli Mwokozi wa ulimwengu."  

 

 

-

43


 

  Baada ya siku mbili Yesu aliondoka hapo, akaenda Galilaya.  

 

 

-

44


 

  Maana Yesu mwenyewe alisema waziwazi kwamba, "Nabii hapati heshima katika nchi yake."  

 

 

-

45


 

  Basi, alipofika Galilaya, Wagalilaya wengi walimkaribisha. Maana nao pia walikuwa kwenye sikukuu ya Pasaka, wakayaona mambo yote Yesu aliyotenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu hiyo.  

 

 

-

46


 

  Yesu alifika tena huko mjini Kana, mkoani Galilaya, mahali alipogeuza maji kuwa divai. Kulikuwa na ofisa mmoja aliyekuwa na mtoto mgonjwa huko Kafarnaumu.  

 

 

-

47


 

  Basi, huyo ofisa aliposikia kuwa Yesu alikuwa ametoka Yudea na kufika Galilaya, alimwendea akamwomba aende kumponya mtoto wake aliyekuwa mgonjwa mahututi.  

 

 

-

48


 

  Yesu akamwambia, "Msipoona ishara na maajabu hamtaamini!"  

 

 

-

49


 

  Huyo ofisa akamwambia, "Mheshimiwa, tafadhali twende kabla mwanangu hajafa."  

 

 

-

50


 

  Yesu akamwambia, "Nenda tu, mwanao yu mzima." Huyo mtu akaamini maneno ya Yesu, akaenda zake.  

 

 

-

51


 

  Alipokuwa bado njiani, watumishi wake walikutana naye, wakamwambia kwamba mwanawe alikuwa mzima.  

 

 

-

52


 

  Naye akawauliza saa mtoto alipopata nafuu; nao wakamwambia, "Jana saa saba mchana, homa ilimwacha."  

 

 

-

53


 

  Huyo baba akakumbuka kwamba ilikuwa ni saa ileile ambapo Yesu alimwambia: "Mwanao yu mzima." Basi, yeye akaamini pamoja na jamaa yake yote.  

 

 

-

54


 

  Hii ilikuwa ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipokuwa anatoka Yudea kwenda Galilaya.  

 

 

-

John 5

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: