Swahili New Testament Bible

John 2

John

Return to Index

Chapter 3

1


 

  Kulikuwa na kiongozi mmoja Myahudi, wa kikundi cha Mafarisayo, jina lake Nikodemo.  

 

 

-

2


 

  Siku moja alimwendea Yesu usiku, akamwambia, "Rabi, tunajua kwamba wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, maana hakuna mtu awezaye kufanya ishara unazozifanya Mungu asipokuwa pamoja naye."  

 

 

-

3


 

  Yesu akamwambia, "Kweli nakwambia, mtu asipozaliwa upya hataweza kuuona ufalme wa Mungu."  

 

 

-

4


 

  Nikodemo akamwuliza, "Mtu mzima awezaje kuzaliwa tena? Hawezi kuingia tumboni mwa mama yake na kuzaliwa mara ya pili!"  

 

 

-

5


 

  Yesu akamjibu, "Kweli nakwambia, mtu asipozaliwa kwa maji na Roho, hawezi kamwe kuingia katika ufalme wa Mungu.  

 

 

-

6


 

  Mtu huzaliwa kimwili kwa baba na mama, lakini huzaliwa kiroho kwa Roho.  

 

 

-

7


 

  Usistaajabu kwamba nimekwambia kuwa ni lazima kuzaliwa upya.  

 

 

-

8


 

  Upepo huvuma kuelekea upendako; waisikia sauti yake, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda. Ndivyo ilivyo kwa mtu aliyezaliwa kwa Roho."  

 

 

-

9


 

  Nikodemo akamwuliza, "Mambo haya yanawezekanaje?"  

 

 

-

10


 

  Yesu akamjibu, "Je, wewe ni mwalimu katika Israel na huyajui mambo haya?  

 

 

-

11


 

  Kweli nakwambia, sisi twasema tunayoyajua na kushuhudia tuliyoyaona, lakini ninyi hamkubali ujumbe wetu.  

 

 

-

12


 

  Ikiwa nimewaambieni mambo ya kidunia nanyi hamniamini, mtawezaje kuamini nikiwaambieni mambo ya mbinguni?  

 

 

-

13


 

  Hakuna mtu aliyepata kwenda juu mbinguni isipokuwa Mwana wa Mtu ambaye ameshuka kutoka mbinguni.  

 

 

-

14


 

  "Kama vile Mose alivyomwinua juu nyoka wa shaba kule jangwani, naye Mwana wa Mtu atainuliwa juu vivyo hivyo,  

 

 

-

15


 

  ili kila anayemwamini awe na uzima wa milele.  

 

 

-

16


 

  Maana Mungu aliupenda ulimwengu hivi hata akamtoa Mwana wake wa pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.  

 

 

-

17


 

  Maana Mungu hakumtuma Mwanae ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali aukomboe ulimwengu.  

 

 

-

18


 

  "Anayemwamini Mwana hahukumiwi; asiyemwamini amekwisha hukumiwa kwa sababu hakumwamini Mwana wa pekee wa Mungu.  

 

 

-

19


 

  Na hukumu yenyewe ndiyo hii: Mwanga umekuja ulimwenguni lakini watu wakapenda giza kuliko mwanga, kwani matendo yao ni maovu.  

 

 

-

20


 

  Kila mtu atendaye maovu anauchukia mwanga, wala haji kwenye mwanga, maana hapendi matendo yake maovu yamulikwe.  

 

 

-

21


 

  Lakini mwenye kuuzingatia ukweli huja kwenye mwanga, ili matendo yake yaonekane yametendwa kwa kumtii Mungu."  

 

 

-

22


 

  Baada ya hayo, Yesu alifika mkoani Yudea pamoja na wanafunzi wake. Alikaa huko pamoja nao kwa muda, akibatiza watu.  

 

 

-

23


 

  Yohane pia alikuwa akibatiza watu huko Ainoni, karibu na Salemu, maana huko kulikuwa na maji mengi. Watu walimwendea, naye akawabatiza.  

 

 

-

24


 

  Wakati huo Yohane alikuwa bado hajafungwa gerezani.)  

 

 

-

25


 

  Ubishi ulitokea kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohane na Myahudi mmoja kuhusu desturi za kutawadha.  

 

 

-

26


 

  Basi, wanafunzi hao wakamwendea Yohane na kumwambia, "Mwalimu, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ng`ambo ya Yordani na ambaye wewe ulimshuhudia, sasa naye anabatiza, na watu wote wanamwendea."  

 

 

-

27


 

  Yohane akawaambia, "Mtu hawezi kuwa na kitu asipopewa na Mungu.  

 

 

-

28


 

  Nanyi wenyewe mwaweza kushuhudia kuwa nilisema: `Mimi siye Kristo, lakini nimetumwa ili nimtangulie!`  

 

 

-

29


 

  Bibiarusi ni wake bwanaarusi, lakini rafiki yake bwana arusi, anayesimama na kusikiliza, hufurahi sana anapomsikia bwana arusi akisema. Ndivyo furaha yangu ilivyokamilishwa.  

 

 

-

30


 

  Ni lazima yeye azidi kuwa maarufu, na mimi nipungue.  

 

 

-

31


 

  "Anayekuja kutoka juu ni mkuu kuliko wote; atokaye duniani ni wa dunia, na huongea mambo ya kidunia. Lakini anayekuja kutoka mbinguni ni mkuu kuliko wote.  

 

 

-

32


 

  Yeye husema yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna mtu anayekubali ujumbe wake.  

 

 

-

33


 

  Lakini mtu yeyote anayekubali ujumbe wake anathibitisha kwamba Mungu ni kweli.  

 

 

-

34


 

  Yule aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, maana Mungu humjalia mtu huyo Roho wake bila kipimo.  

 

 

-

35


 

  Baba anampenda Mwana na amemkabidhi vitu vyote.  

 

 

-

36


 

  Anayemwamini Mwana anao uzima wa milele; asiyemtii Mwana hatakuwa na uzima wa milele, bali ghadhabu ya Mungu hubaki juu yake."  

 

 

-

John 4

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: