Swahili New Testament Bible

Luke 23

Luke

Return to Index

Chapter 24

1


 

  Jumapili, alfajiri na mapema, wale wanawake walikwenda kaburini wakichukua yale manukato waliyotayarisha.  

 

 

-

2


 

  Walikuta lile jiwe limeviringishwa mbali na kaburi.  

 

 

-

3


 

  Walipoingia ndani, hawakuona mwili wa Bwana Yesu.  

 

 

-

4


 

  Walipokuwa bado wanashangaa juu ya jambo hilo, mara watu wawili waliovaa mavazi yenye kung`aa sana, wakasimama karibu nao.  

 

 

-

5


 

  Hao wanawake wakaingiwa na hofu, wakainama chini. Ndipo wale watu wakawaambia, "Kwa nini mnamtafuta aliye hai kati ya wafu?  

 

 

-

6


 

  Hayuko hapa; amefufuka. Kumbukeni aliyowaambieni alipokuwa kule Galilaya:  

 

 

-

7


 

  `Ni lazima Mwana wa Mtu atolewe kwa watu waovu, nao watamsulubisha, na siku ya tatu atafufuka."`  

 

 

-

8


 

  Hapo wanawake wakayakumbuka maneno yake,  

 

 

-

9


 

  wakarudi kutoka kaburini, wakawapa mitume wale kumi na mmoja na wengine habari za mambo hayo yote.  

 

 

-

10


 

  Hao waliotoa habari hizo kwa mitume ni: Maria Magdalene, Yoana na Maria mama wa Yakobo, pamoja na wanawake wengine walioandamana nao.  

 

 

-

11


 

  Mitume waliyachukua maneno hayo kama yasiyo na msingi, hivyo hawakuamini.  

 

 

-

12


 

  Lakini Petro alitoka, akaenda mbio hadi kaburini. Alipoinama kuchungulia ndani, akaiona tu ile sanda. Akarudi nyumbani huku akiwa anashangaa juu ya hayo yaliyotokea.  

 

 

-

13


 

  Siku hiyohiyo, wawili kati ya wafuasi wake Yesu wakawa wanakwenda katika kijiji kimoja kiitwacho Emau, umbali wa kilomita kumi na moja kutoka Yerusalemu.  

 

 

-

14


 

  Wakawa wanazungumza juu ya hayo yote yaliyotukia.  

 

 

-

15


 

  Walipokuwa wakizungumza na kujadiliana, Yesu mwenyewe akatokea, akatembea pamoja nao.  

 

 

-

16


 

  Walimwona kwa macho, lakini hawakumtambua.  

 

 

-

17


 

  Akawauliza, "Mnazungumza nini huku mnatembea?" Nao wakasimama kimya, nyuso zao wamezikunja kwa huzuni.  

 

 

-

18


 

  Mmoja, aitwaye Kleopa, akamjibu, "Je, wewe ni mgeni peke yako Yerusalemu ambaye hujui yaliyotukia huko siku hizi?"  

 

 

-

19


 

  Naye akawajibu, "Mambo gani?" Wao wakamjibu, "Mambo yaliyompata Yesu wa Nazareti. Yeye alikuwa nabii mwenye uwezo wa kutenda na kufundisha mbele ya Mungu na mbele ya watu wote.  

 

 

-

20


 

  Makuhani na watawala wetu walimtoa ahukumiwe kufa, wakamsulubisha.  

 

 

-

21


 

  Lakini sisi tulitumaini kwamba yeye ndiye angeikomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu mambo hayo yalipotendeka.  

 

 

-

22


 

  Tena, wanawake wengine wa kwetu wametushtua. Walikwenda kaburini mapema asubuhi,  

 

 

-

23


 

  wasiukute mwili wake. Wakarudi wakasema kwamba walitokewa na malaika waliowaambia kwamba alikuwa hai.  

 

 

-

24


 

  Wengine wetu walikwenda kaburini wakashuhudia yale waliyosema hao wanawake; ila yeye hawakumwona."  

 

 

-

25


 

  Kisha Yesu akawaambia, "Mbona mu wapumbavu kiasi hicho na mioyo yenu ni mizito hivyo kusadiki yote yaliyonenwa na manabii?  

 

 

-

26


 

  Je, haikumpasa Kristo kuteswa, na hivyo aingie katika utukufu wake?"  

 

 

-

27


 

  Akawafafanulia mambo yote yaliyomhusu yeye katika Maandiko Matakatifu kuanzia Mose hadi manabii wote.  

 

 

-

28


 

  Walipokikaribia kile kijiji walikokuwa wanakwenda, Yesu akafanya kana kwamba anaendelea na safari;  

 

 

-

29


 

  lakini wao wakamsihi wakisema, "Kaa pamoja nasi, maana kunakuchwa, na usiku unakaribia." Basi, akaingia kijijini, akakaa pamoja nao.  

 

 

-

30


 

  Alipoketi kula chakula pamoja nao, akachukua mkate, akaubariki, akaumega, akawapa.  

 

 

-

31


 

  Mara macho yao yakafumbuliwa, wakamtambua; lakini yeye akatoweka kati yao.  

 

 

-

32


 

  Basi, wakaambiana, "Je, mioyo yetu haikuwa inawaka ndani yetu wakati alipokuwa anatufafanulia Maandiko Matakatifu kule njiani?"  

 

 

-

33


 

  Wakaondoka saa ileile, wakarudi Yerusalemu: wakawakuta wale mitume kumi na mmoja na wale wengine waliokuwa pamoja nao, wamekusanyika  

 

 

-

34


 

  wakisema, "Hakika Bwana amefufuka, amemtokea Simoni."  

 

 

-

35


 

  Basi, hao wafuasi wawili wakawajulisha yale yaliyowapata njiani, na jinsi walivyomtambua katika kumega mkate.  

 

 

-

36


 

  Wanafunzi wote wawili walipokuwa wakiwaambia hayo, Yesu mwenyewe akasimama kati yao, akawaambia "Amani kwenu."  

 

 

-

37


 

  Wakashtuka na kushikwa na hofu wakidhani wameona mzimu.  

 

 

-

38


 

  Lakini yeye akawaambia, "Kwa nini mnafadhaika? Mbona mnakuwa na mashaka mioyoni mwenu?  

 

 

-

39


 

  Angalieni mikono na miguu yangu, ya kwamba ni mimi mwenyewe. Nipapaseni mkanione, maana mzimu hauna mwili na mifupa kama mnionavyo."  

 

 

-

40


 

  Baada ya kusema hayo, akawaonyesha mikono na miguu.  

 

 

-

41


 

  Wakiwa bado katika hali ya kutosadiki kwa sababu ya furaha yao, na wakiwa wanastaajabu, akawauliza, "Mnacho chakula chochote hapa?"  

 

 

-

42


 

  Wakampa kipande cha samaki wa kuokwa.  

 

 

-

43


 

  Akakichukua, akala, wote wakimwona.  

 

 

-

44


 

  Halafu akawaambia, "Hii ndiyo maana ya maneno niliyowaambia nilipokuwa pamoja nanyi: kwamba ilikuwa lazima kukamilisha yote yaliyoandikwa juu yangu katika Sheria ya Mose na katika vitabu vya manabii na katika kitabu cha Zaburi."  

 

 

-

45


 

  Kisha, akaziangazia akili zao ili wapate kuelewa Maandiko Matakatifu.  

 

 

-

46


 

  Akawaambia, "Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka wafu,  

 

 

-

47


 

  na kwamba ni lazima, kwa jina lake, mataifa yote kuanzia na Yerusalemu yahubiriwe juu ya kutubu na kusamehewa dhambi.  

 

 

-

48


 

  Ninyi ni mashahidi wa mambo hayo.  

 

 

-

49


 

  Nami mwenyewe nitawapelekeeni yule ambaye Baba aliahidi kumtuma, lakini ngojeni huku mjini mpaka mtakapopewa ile nguvu itokayo juu."  

 

 

-

50


 

  Kisha akawaongoza nje ya mji hadi Bethania, akainua mikono yake juu, akawabariki.  

 

 

-

51


 

  Alipokuwa anawabariki, akawaacha; akachukuliwa mbinguni.  

 

 

-

52


 

  Wao wakamwabudu, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kubwa:  

 

 

-

53


 

  wakakaa muda wote Hekaluni wakimsifu Mungu.  

 

 

-

John 1

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: