Swahili New Testament Bible

Luke 20

Luke

Return to Index

Chapter 21

1


 

  Yesu alitazama kwa makini, akawaona matajiri walivyokuwa wanatia sadaka zao katika hazina ya Hekalu,  

 

 

-

2


 

  akamwona pia mama mmoja mjane akitumbukiza humo sarafu mbili ndogo.  

 

 

-

3


 

  Basi, akasema, "Nawaambieni kweli, mama huyu mjane ametia zaidi katika hazina kuliko wote.  

 

 

-

4


 

  Kwa maana, wengine wote wametoa sadaka zao kutokana na ziada ya mali zao, lakini huyu mama, ingawa ni maskini, ametoa kila kitu alichohitaji kwa kuishi."  

 

 

-

5


 

  Baadhi ya wanafunzi walikuwa wanazungumza juu ya Hekalu, jinsi lilivyopambwa kwa mawe ya thamani, pamoja na sadaka zilizotolewa kwa Mungu. Yesu akasema,  

 

 

-

6


 

  "Haya yote mnayoyaona--zitakuja siku ambapo hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa."  

 

 

-

7


 

  Basi, wakamwuliza, "Mwalimu, mambo hayo yatatokea lini? Na ni ishara gani zitakazoonyesha kwamba karibu mambo hayo yatokee?"  

 

 

-

8


 

  Yesu akawajibu, "Jihadharini, msije mkadanganyika. Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: `Mimi ndiye`, na, `Wakati ule umekaribia`. Lakini ninyi msiwafuate!  

 

 

-

9


 

  Basi, mtakaposikia habari za vita na misukosuko, msitishike; maana ni lazima hayo yatokee kwanza, lakini mwisho wa yote, bado."  

 

 

-

10


 

  Halafu akaendelea kusema: "Taifa moja litapigana na taifa lingine, na ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine.  

 

 

-

11


 

  Kila mahali kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, kutakuwa na njaa na tauni. Kutakuwa na vituko vya kutisha na ishara kubwa angani.  

 

 

-

12


 

  Lakini kabla ya kutokea hayo yote, watawatieni nguvuni, watawatesa na kuwapelekeni katika masunagogi na kuwatia gerezani; mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya jina langu.  

 

 

-

13


 

  Hii itawapeni fursa ya kushuhudia Habari Njema.  

 

 

-

14


 

  Muwe na msimamo huu mioyoni mwenu: hakuna kufikiria kabla ya wakati juu ya jinsi mtakavyojitetea,  

 

 

-

15


 

  kwa sababu mimi mwenyewe nitawapeni ufasaha wa maneno na hekima, hivyo kwamba zenu hawataweza kustahimili wala kupinga.  

 

 

-

16


 

  Wazazi wenu, ndugu, jamaa na rafiki zenu watawasaliti ninyi; na baadhi yenu mtauawa.  

 

 

-

17


 

  Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu.  

 

 

-

18


 

  Lakini, hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.  

 

 

-

19


 

  Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.  

 

 

-

20


 

  "Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo mtambue ya kwamba wakati umefika ambapo mji huo utaharibiwa.  

 

 

-

21


 

  Hapo walioko Yudea wakimbilie milimani; wale walio mjini watoke; na wale walio mashambani wasirudi mjini.  

 

 

-

22


 

  Kwa maana siku hizo ni siku za adhabu, ili yote yaliyoandikwa yatimie.  

 

 

-

23


 

  Ole wao waja wazito na wanyonyeshao siku hizo! Kwa maana kutakuwa na dhiki kubwa katika nchi, na hasira ya Mungu itawajia watu hawa.  

 

 

-

24


 

  Wengine watauawa kwa upanga, wengine watachukuliwa mateka katika nchi zote; na mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa mataifa mengine, hadi nyakati zao zitakapotimia.  

 

 

-

25


 

  "Kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota. Mataifa duniani yatakuwa na dhiki kwa sababu ya wasiwasi kutokana na mshindo wa mawimbi ya bahari.  

 

 

-

26


 

  Watu watazirai kwa sababu ya uoga, wakitazamia mambo yatakayoupata ulimwengu; kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.  

 

 

-

27


 

  Halafu, watamwona Mwana wa Mtu akija katika wingu, mwenye nguvu na utukufu mwingi.  

 

 

-

28


 

  Wakati mambo hayo yatakapoanza kutukia, simameni na kuinua vichwa vyenu juu, kwa maana ukombozi wenu umekaribia."  

 

 

-

29


 

  Kisha akawaambia mfano: "Angalieni mtini na miti mingine yote.  

 

 

-

30


 

  Mnapoona kwamba imeanza kuchipua majani, mwatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.  

 

 

-

31


 

  Vivyo hivyo, mtakapoona mambo hayo yanatendeka, mtatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.  

 

 

-

32


 

  Nawaambieni hakika, kizazi hiki cha sasa hakitapita kabla ya hayo yote kutendeka.  

 

 

-

33


 

  Mbingu na dunia vitapita, lakini maneno yangu hayatapita.  

 

 

-

34


 

  "Muwe macho, mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na shughuli za maisha haya. La sivyo, Siku ile itawajieni ghafla.  

 

 

-

35


 

  Kwa maana itawajia kama mtego, wote wanaoishi duniani pote.  

 

 

-

36


 

  Muwe waangalifu basi, na salini daima ili muweze kupata nguvu ya kupita salama katika mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Mtu."  

 

 

-

37


 

  Wakati wa mchana, siku hizo, Yesu alikuwa akifundisha watu Hekaluni; lakini usiku alikuwa akienda katika mlima wa Mizeituni na kukaa huko.  

 

 

-

38


 

  Watu wote walikuwa wanakwenda Hekaluni asubuhi na mapema, wapate kumsikiliza.  

 

 

-

Luke 22

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: