Swahili New Testament Bible

Matthew 22

Matthew

Return to Index

Chapter 24

1


 

  Yesu alitoka Hekaluni, na alipokuwa akienda zake, wanafunzi wake walimwendea, wakamwonyesha majengo ya Hekalu.  

 

 

-

2


 

  Yesu akawaambia, "Sawa, mnaweza kuyatazama haya yote! Kweli nawaambieni, hakuna hata jiwe moja litakalosalia hapa juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa."  

 

 

-

3


 

  Yesu alipokuwa ameketi juu ya mlima wa Mizeituni, wanafunzi walimwendea faraghani, wakamwuliza, "Twambie mambo haya yatatukia lini? Ni ishara gani itakayoonyesha kuja kwako na mwisho wa nyakati?"  

 

 

-

4


 

  Yesu akawajibu, "Jihadharini msije mkadanganywa na mtu.  

 

 

-

5


 

  Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: `Mimi ndiye Kristo,` nao watawapotosha watu wengi.  

 

 

-

6


 

  Mtasikia juu ya vita na fununu za vita; lakini msifadhaike, maana hayo hayana budi kutokea, lakini mwisho wenyewe ungali bado.  

 

 

-

7


 

  Taifa moja litapigana na taifa lingine; ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine. Hapa na pale patakuwa na njaa na mitetemeko ya ardhi.  

 

 

-

8


 

  Yote hayo ni kama mwanzo wa maumivu ya kujifungua mtoto.  

 

 

-

9


 

  "Kisha watawatoeni ili mteswe na kuuawa. Mataifa yote yatawachukieni kwa ajili ya jina langu.  

 

 

-

10


 

  Tena, wengi wataiacha imani yao, watasalitiana na kuchukiana.  

 

 

-

11


 

  Watatokea manabii wengi wa uongo watakaowapotosha watu wengi.  

 

 

-

12


 

  Kwa sababu ya ongezeko la uhalifu, upendo wa watu wengi utafifia.  

 

 

-

13


 

  Lakini atakayevumilia mpaka mwisho, ataokoka.  

 

 

-

14


 

  Ila, kabla ya mwisho kufika, hii Habari Njema ya Ufalme wa Mungu itahubiriwa ulimwenguni kote kama ushuhuda kwa mataifa yote.  

 

 

-

15


 

  "Basi, mtakapoona `Chukizo Haribifu` lililonenwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu, (msomaji na atambue maana yake),  

 

 

-

16


 

  hapo, walioko Yudea na wakimbilie milimani.  

 

 

-

17


 

  Aliye juu ya paa la nyumba yake asishuke kuchukua kitu nyumbani mwake.  

 

 

-

18


 

  Aliye shambani asirudi nyuma kuchukua vazi lake.  

 

 

-

19


 

  Ole wao kina mama waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo!  

 

 

-

20


 

  Ombeni ili kukimbia kwenu kusiwe siku za baridi au siku ya Sabato!  

 

 

-

21


 

  Maana wakati huo kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka leo, wala haitapata kutokea tena.  

 

 

-

22


 

  Kama siku hizo hazingalipunguzwa, hakuna binadamu yeyote ambaye angeokoka; lakini siku hizo zitapunguzwa kwa ajili ya wale walioteuliwa.  

 

 

-

23


 

  "Basi, mtu akiwaambieni siku hizo: `Kristo yuko hapa` au `Yuko pale,` msimsadiki.  

 

 

-

24


 

  Maana watatokea kina Kristo wa uongo na manabii wa uongo. Watafanya ishara kubwa na maajabu ya kuweza kuwapotosha ikiwezekana hata wateule wa Mungu.  

 

 

-

25


 

  Sikilizeni, nimekwisha kuwaonya kabla ya wakati.  

 

 

-

26


 

  Basi, wakiwaambieni, `Tazameni, yuko jangwani,` msiende huko; au, `Tazameni, amejificha ndani,` msisadiki;  

 

 

-

27


 

  maana, kama vile umeme uangazavyo toka mashariki hadi magharibi, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Mtu.  

 

 

-

28


 

  Pale ulipo mzoga, ndipo watakapokusanyika tai.  

 

 

-

29


 

  "Mara baada ya dhiki ya siku hizo, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza, nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za mbingu zitatikiswa.  

 

 

-

30


 

  Kisha, ishara ya Mwana wa Mtu itaonekana angani, na hapo makabila yote duniani yatalalamika; watamwona Mwana wa Mtu akija juu ya mawingu ya angani mwenye nguvu na utukufu mwingi.  

 

 

-

31


 

  Naye atawatuma malaika wake wenye tarumbeta la kuvuma sana, nao watawakusanya wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, toka mwisho huu wa mbingu hadi mwisho huu.  

 

 

-

32


 

  "Kwa mtini jifunzeni mfano huu: Mara tu matawi yake yanapoanza kuwa laini na kuchanua majani, mnajua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.  

 

 

-

33


 

  Hali kadhalika nanyi mtakapoona mambo haya yote yakitendeka, jueni kwamba yuko karibu sana.*fk*  

 

 

-

34


 

  Nawaambieni kweli, kizazi hiki hakitapita kabla ya mambo hayo yote kutukia.  

 

 

-

35


 

  Naam, mbingu na dunia zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.  

 

 

-

36


 

  "Lakini, juu ya siku au saa hiyo, hakuna mtu ajuaye itakuja lini; wala malaika wa mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake ndiye ajuaye.  

 

 

-

37


 

  Kwa maana kama ilivyokuwa nyakati za Noa, ndivyo itakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Mtu.  

 

 

-

38


 

  Maana nyakati hizo, kabla ya gharika kuu, watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka Noa alipoingia ndani ya ile safina.  

 

 

-

39


 

  Hawakujua kuna nini mpaka ile gharika ilipotokea, ikawakumba wote. Ndivyo itakavyokuwa wakati Mwana wa Mtu atakapokuja.  

 

 

-

40


 

  Wakati huo watu wawili watakuwa shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.  

 

 

-

41


 

  Kina mama wawili watakuwa wanasaga nafaka, mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.  

 

 

-

42


 

  Basi, kesheni, kwa maana hamjui siku atakayokuja Bwana wenu.  

 

 

-

43


 

  Lakini kumbukeni jambo hili: kama mwenye nyumba angejua siku mwizi atakapofika, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.  

 

 

-

44


 

  Kwa hiyo, nanyi pia muwe tayari, kwa maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia."  

 

 

-

45


 

  Yesu akaendelea kusema, "Ni nani basi mtumishi mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watu wake, awape chakula kwa wakati wake?  

 

 

-

46


 

  Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakapokuja atamkuta akifanya hivyo.  

 

 

-

47


 

  Kweli nawaambieni, atamweka mtumishi huyo aisimamie mali yake yote.  

 

 

-

48


 

  Lakini kama mtumishi mbaya akijisemea moyoni: `Bwana wangu anakawia kurudi,`  

 

 

-

49


 

  kisha akaanza kuwapiga watumishi wenzake, akaanza kula na kunywa pamoja na walevi,  

 

 

-

50


 

  bwana wake atakuja siku asiyoitazamia na saa asiyoijua.  

 

 

-

51


 

  Atamkatilia mbali na kumweka kundi moja na wanafiki. Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.  

 

 

-

Matthew 25

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: