Swahili New Testament Bible

Matthew 14

Matthew

Return to Index

Chapter 15

1


 

  Kisha Mafarisayo na walimu wa Sheria wakafika kutoka Yerusalemu, wakamwendea Yesu, wakamwuliza,  

 

 

-

2


 

  "Kwa nini wanafunzi wako hawajali mapokeo tuliyopokea kutoka kwa wazee wetu? Hawanawi mikono yao kama ipasavyo kabla ya kula!"  

 

 

-

3


 

  Yesu akawajibu, "Kwa nini nanyi mnapendelea mapokeo yenu wenyewe na hamuijali Sheria ya Mungu?  

 

 

-

4


 

  Mungu amesema: `Waheshimu baba yako na mama yako,` na `Anayemkashifu baba yake au mama yake, lazima auawe`.  

 

 

-

5


 

  Lakini ninyi mwafundisha ati mtu akiwa na kitu ambacho angeweza kuwasaidia nacho baba au mama yake, lakini akasema: `Kitu hiki nimemtolea Mungu,`  

 

 

-

6


 

  basi, hapaswi tena kumheshimu baba yake! Ndivyo mnavyodharau neno la Mungu kwa kufuata mafundisho yenu wenyewe.  

 

 

-

7


 

  Enyi wanafiki! Isaya alitabiri sawa kabisa juu yenu:  

 

 

-

8


 

  `Watu hawa, asema Mungu, huniheshimu kwa maneno tu, lakini mioyoni mwao wako mbali nami.  

 

 

-

9


 

  Kuniabudu kwao hakufai, maana mambo wanayofundisha ni maagizo ya kibinadamu tu."`  

 

 

-

10


 

  Yesu aliuita ule umati wa watu, akawaambia, "Sikilizeni na muelewe!  

 

 

-

11


 

  Kitu kinachomtia mtu najisi si kile kiingiacho kinywani, bali kile kitokacho kinywani. Hicho ndicho kimtiacho mtu najisi."  

 

 

-

12


 

  Kisha wanafunzi wakamwendea, wakamwambia, "Je, unajua kwamba Mafarisayo walichukizwa waliposikia maneno yako?"  

 

 

-

13


 

  Lakini yeye akawajibu, "Kila mmea ambao Baba yangu aliye mbinguni hakuupanda, utang`olewa.  

 

 

-

14


 

  Waacheni wenyewe! Wao ni vipofu, viongozi wa vipofu; na kipofu akimwongoza kipofu, wote wawili hutumbukia shimoni."  

 

 

-

15


 

  Petro akadakia, "Tufafanulie huo mfano."  

 

 

-

16


 

  Yesu akasema, "Hata nyinyi hamwelewi?  

 

 

-

17


 

  Je, hamwelewi kwamba kila kinachoingia kinywani huenda tumboni na baadaye hutupwa nje chooni?  

 

 

-

18


 

  Lakini yale yatokayo kinywani hutoka moyoni, na hayo ndiyo yanayomtia mtu najisi.  

 

 

-

19


 

  Maana moyoni hutoka mawazo maovu yanayosababisha uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushahidi wa uongo na kashfa.  

 

 

-

20


 

  Hayo ndiyo yanayomtia mtu najisi. Lakini kula chakula bila kunawa mikono hakumtii mtu najisi."  

 

 

-

21


 

  Yesu aliondoka mahali hapo akaenda kukaa katika sehemu za Tiro na Sidoni.  

 

 

-

22


 

  Basi, mama mmoja Mkaanani wa nchi hiyo alimjia, akapaaza sauti: "Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, nionee huruma! Binti yangu anasumbuliwa na pepo."  

 

 

-

23


 

  Lakini Yesu hakumjibu neno. Basi, wanafunzi wake wakamwendea, wakamwambia, "Mwambie aende zake kwa maana anatufuatafuata akipiga kelele."  

 

 

-

24


 

  Yesu akajibu, "Sikutumwa ila kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo."  

 

 

-

25


 

  Hapo huyo mama akaja, akapiga magoti mbele yake, akasema, "Mheshimiwa, nisaidie."  

 

 

-

26


 

  Yesu akamjibu, "Si sawa kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa."  

 

 

-

27


 

  Huyo mama akajibu, "Ni kweli, Mheshimiwa; lakini hata mbwa hula makombo yanayoanguka kutoka meza ya bwana wao."  

 

 

-

28


 

  Hapo Yesu akamjibu, "Mama, imani yako ni kubwa; basi, ufanyiwe kama unavyotaka." Yule binti yake akapona tangu saa hiyo wakati huohuo.  

 

 

-

29


 

  Yesu alitoka hapo akaenda kando ya ziwa Galilaya, akapanda mlimani, akaketi.  

 

 

-

30


 

  Watu wengi sana wakamjia wakiwaleta vilema, vipofu, viwete, bubu na wengine wengi waliokuwa wagonjwa, wakawaweka mbele ya miguu yake, naye Yesu akawaponya.  

 

 

-

31


 

  Umati ule wa watu ulishangaa sana ulipoona bubu wakiongea, waliokuwa wamelemaa wamepona, viwete wakitembea na vipofu wakiona; wakamsifu Mungu wa Israeli.  

 

 

-

32


 

  Basi, Yesu aliwaita wanafunzi wake, akasema, "Nawaonea watu hawa huruma kwa sababu kwa siku tatu wamekuwa nami, wala hawana chakula. Sipendi kuwaacha waende bila kula wasije wakazimia njiani."  

 

 

-

33


 

  Wanafunzi wakamwambia, "Hapa tuko nyikani; tutapata wapi chakula cha kuwatosha watu wengi hivi?"  

 

 

-

34


 

  Yesu akawauliza, "Mnayo mikate mingapi?" Wakamjibu, "Saba na visamaki vichache."  

 

 

-

35


 

  Basi, Yesu akawaamuru watu wakae chini.  

 

 

-

36


 

  Akaitwaa ile mikate saba na vile visamaki, akamshukuru Mungu, akavimega, akawapa wanafunzi, nao wakawagawia watu.  

 

 

-

37


 

  Wote wakala, wakashiba. Kisha wakakusanya makombo, wakajaza vikapu saba.  

 

 

-

38


 

  Hao waliokula walikuwa wanaume elfu nne, bila kuhesabu wanawake na watoto.  

 

 

-

39


 

  Basi, Yesu akawaaga watu, akapanda mashua, akaenda katika eneo la Magadani.  

 

 

-

Matthew 16

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: